Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Habari la Hawza, Ustadh Shahidi Murtadha Mutahhari katika moja ya maandiko yake amezungumzia mada ya “Mbinu ya kipekee ya Uislamu kwa kupambana na dhalimu” ambayo inawasilishwa kwenu kama ifuatavyo.
Je, Uislamu umemwambia dhalimu tu: Ewe dhalimu! Usidhulumu? Je, madhalimu wote husikia?
Wapo waovu wengi lakini hawasikii.
Basi Uislamu hufanya nini kingine?
Huondoa mazingira ya kukubali dhulma pia.
Humwambia aliyedhulumiwa: "Ewe uliyedhulumiwa! Kukubali dhulma ni aina ya kudhulumu, simama dhidi ya dhalimu na paza sauti."
"لایحِبُّ اللهُ الْجَهْرَ بِالسّوءِ مِنَ الْقَوْلِ الّا مَنْ ظُلِمَ"
Mwenyezi Mungu hapendi kupaza sauti kwa maneno maovu, isipokuwa kwa yule ambaye amedhulumiwa.
Qur’an inasema kwamba kusema mabaya nyuma ya mgongo wa Muislamu [yaani kufichua maovu yake] ni jambo baya, na baya zaidi ni pale mtu anapopaza sauti anaposema mabaya.
Lakini ubaya huu katika hali moja unaruhusiwa.
Yaani: Sema mabaya! Paza sauti!
Dai haki yako pale unapodhulumiwa.
Chanzo: Kitabu cha “Kumi na Tano Hotuba”, uk. 263 (kwa muhtasari)
Maoni yako